TRAFIKI KUVAA NEPI WAKATI WA ZIARA YA PAPA FRANCIS

Wakati Papa Francis atakapoitembelea Ufilipino wiki ijayo, askari wa barabarani(trafiki) hawatokubali mitaa ya mji mkuu kufungwa na kuwa na msongamano mkubwa endapo watatakiwa kufanya hivyo.

Askari zaidi ya 2,000 ambao watakuwa na zamu siku za Januari 15-19 kwenye ziara ya Papa watatakiwa kuvaa nepi za watoto (diapes), alisema Francis Tolentino, mwenyekiti wa Uongozi wa Maendeleo ya Metropolitan jijini Manila.

Tolentino pia aliwahamasisha watu ambao watamsubiria kwa masaa kumuona Papa pia wavae nepi.

Zoezi la kuvaa nepi siku ya zamu lilipokelewa vema na watu wake, alisema siku ya Jumatano.

Itakuwa mara ya kwanza kwa askari wa barabarani nchini Ufilipino kuvaa nepi wakiwa kazini mitaani, alisema.

Alipouliza kuwa naye atavaa, Tolentino alisema, "Nitajaribu, ila kwa upande wangu, nina tatizo la kuharisha kidogo."