WAFUKUA NA KUBEBA MWILI WA MAREHEMU NA KUTOKOMEA NAO

Watu wasiofahamika wamefukua kabuli na kubeba mwili wa marehemu aliyekuwa amezikwa kwenye makaburi ya Isanjandugu Tarafa ya Nsimbo Wilaya ya Mlele Mkoani Katavi kwa kile kinachodaiwa kuwa ni imani za kishirikina Kwa mujibu wa Diwani wa Kata ya Nsimbo Michael Kasanga(CCM) alisema tukio hilo la imani za kishilikina lilitokea hapo juzi kwenye makaburi ya Isanjandugu Tarafa ya Nsimbo.

Alisema kabuli la marehemu huyo ambalo lilifukuliwa na watu wasiojulikana liligunduliwa hapo juzi na wananchi wawili waliokuwa wanakwenda shambani ambao walipita jirani na makabuli hayo na kuona kabuli hilo limefukuliwa.

Diwani Kasanga alieleza baada ya wananchi hao wawili kuona kabuli hilo limefukuliwa walishitushwa na hari hiyo na iliwalazimu kurudi kijijini na kutoa taarifa kwa uongozi wa serikali ya kijiji.

Alisema baada ya viongozi wa Kijiji hicho kupata taarifa hiyo waliongozana na baadhi ya wananchi kwenda kwenye maeneo hayo ya makaburi ya Kijiji hicho.

Baada ya kufika kwenye eneo hilo la kabuli hilo walikuta limefukuliwa na watu ambao hawajafamika huku mabaki ya mwili wa marehemu huyo yakiwa yamebebwa kwa kile kinachoonekana ni imani za kishirikina.

Alisema kabuli hilo lilishindwa kufahamika jina la marehemu aliyekuwa amezikwa kwenye kabuli hilo kutona na kile kilichoonekana kuwa kabuli hilo lilikuwa ni la muda mrefu.

Diwani Kasanga alifafanua kuwa imekuwa ni tabia ya muda mrefu kwa wananchi wa Kijiji hicho kuwa na tabia ya kwenda kwenye makabuli hayo mida ya usiku na kuoga dawa za kienyeji juu ya makabuli kwa imani za kishilikina

Alisema anatowa wito kwa wananchi wa Kijiji hicho kuacha tabia hiyo ya kuchezea kwenye makabuli na kuogea dawa kwani tabia hiyo ya imani potofu sio nzuri kwenye jamii.