WANALENGA KUNICHAFUA KISIASA - MH. PINDA

Mh. Pinda ameyasema hayo jana wakati akiwahutubia wananchi wa Mkoa wa Katavi katika Hlamshauri ya mpanda katika mkutano wa hadhara ulifanyika mkoani humu nakuongeza kuwa kama angekuwa fisadi basi angekua mmoja wa matajiri wakubwa nchini.

Mh. Pinda amesema kuwa kama kuna mtu mwenye ushahidi wa yeye kufisadi apeleke kwenye vyombo vya dola ili ashughulikiwe kwa mujibu wa sheria na yupo tayari kufungwa endapo ikithibitika kuwa ni fisadi.

Waziri mkuu ameongeza kuwa hatua hyio ya kumchafua inakuja wakti ambapo ametangaza nia ya Urais na kuongeza kuwa kama kuna mtu alikua na ushahidi wa kutosha dhidi ya upataji wake wa pesa amripoti takukuru ili achukuliwe hatua kwani yupo tayari kufungwa.

Aidha Waziri mkuu amepuuza kauli za baadhi ya watu wanaosema kuwa hana maamuzi katika serikali zaidi ya kulialia na kusisitiza kuwa kazi anayoifanya ni kubwa na inayozingatia msingi ya utawala bora na yenye maadili kiutendaji nakama kuna mapungufu wananchi ndio watakaopima na kutoa maamuzi.