SOMALIA YAPIGA MARUFUKU LUGHA ZA KIGENI

Rais wa Somalia amepiga marufuku ya matumizi ya lugha za kigeni katika ofisi za serikali na kusema kuwa lugha pekee ya mawasiliano katika ofisi hizo ni kisomali.

Rais Hassan Shaykh Mahmud alikuwa akizungumza hayo katika sherehe za maadhimisho ya kutimiza miaka 42 tangu kuanza kutumika kwa lugha ya Kisomali nchini humo ,maadhimisho yaliyofanywa mjini Mogadishu kwa lengo la kutaka kuiimarisha lugha hiyo.

Hata hivyo maadhimisho hayo yalihudhuriwana mamabalozi wanaowakilisha nchi zao nchini humo.

Matumizi ya lugha ya kisomali katika ofisi za serikali yametakiwa kuanza January mosi mwaka huu na kuendelea.

Shughuli zote za kiserikali nchini humo zimetakiwa kuendeshwa katika lugha ya kisomali na si lugha ingine yoyote.

Ruhusa ya matumizi ya lugha za kigeni imetolewa tu wakati wageni kutoka nje ya somalia watakapo kuwa wakihudumiwa.

Hata hivyo waziri wa habari wa taifa hilo,ametilia mkazo kauli hiyo na kudai kwamba January 21 ni siku muhimu sana kwa taifa hilo,na siku hiyo ni kumbu kumbu kwa gazeti la kisomali la kwanza kuchapishwa.

Naye spika wa bunge la Somalia,Muhammad Shaykh Usman Jawari, ambaye pia alitoa kauli yake kwenye maadhimisho hayo,na kusema kwamba ni jambo muhimu kwa jamii ya wasomali kuelewa umuhimu wa lugha yao na kuitaka jamii kuiimarisha lugha hiyo.

Rais Mahmud aliongeza kusema kwamba tarehe 21 January ni siku muhimu kwa wasomali na serikali yao.