DIWANI KUMLIPIA PINDA FOMU YA URAIS

Diwani wa Kata ya Makanyagio (CHADEMA) katika Halmashauri ya Mjiwa Mpanda Idd Nzguye amemwahidi Waziri Mkuu Mizengo kuwa atamlipia pesa za gharama za kuchukulia fomu za kugombea Urais Nzguye alitowa ahadi hiyo mbele ya Waziri Mkuu Mizengo Pinda wakati wa sherehe za kuuwaga mwaka 2014 na kuukaribisha mwaka 2015 zilizofanyika katika Hotel ya Lyamba lyamfipa mjini hapa.

Alisema kuwa ameridhishwa na utendaji wake wa kazi hivyo utakapofikia kipindi cha kuchukua fomu za kugombea Urais gharama ya fomu za kugombea Urais atalipa yeye Diwani Nzguye Alieleza mbele ya umati wa watu waliohudhuria sherehe hizo kuwa Mizigo Pinda anaishi kwenye Kata yakeya Makanyagio hivyo yeye kama Diwani wa Kata hiyo ameamua kutoa ahadi ya kulimpia gharama za pesa za kuchukilia fomu za kugombea Urais Alisema ni jambo la kujivunia kwake kuona mgombea Urais anatoka kwenye kata yake anayoiongoza hivyo ni wajibu wake kumsaidia wananchi wake huyo ambae ni Pinda.

Alisema sababu nyingine iliyomvutia mpaka afikie uamuzi huo wa kumwahidi kulipia fomu ya kugombea Urais ni jinsi ambavyo Pinda hakuusika kabisa na tuhuma za kuchota fedha za IPTL.

Nzguye alisema haoni sababu yoyote ya kutomlipia fomu za kugombea Urais kutokana najitihada zinazofanywa na Pinda za kusimamia shughuli za Serikali.