ATUPWA JELA MAISHA KWA KULAWITI

Kijana mmoja aitwaye Michael Edward (25) mkazi wa Mtaa wa Mji wa Zamani, Mkoa wa Katavi amehukumiwa kifungo cha maisha jela baada ya kupatikana na hatia ya kumbaka na kumlawiti mtoto wa kiume mwenye umri wa miaka saba.

Hukumu hiyo iliyovuta hisia za watu wengi mjini Mpanda, ilitolewa na Hakimu mkazi Mfawidhi wa Mahakama ya Wilaya ya Mpanda, Chiganga Ntengwa baada ya Mahakama kuridhika na ushahidi uliotolewa mahakamani hapo wa pande zote mbili.

Awali, akisoma maelezo ya upande wa mashtaka Mwendesha Mashtaka, Kulwa Sikwesa alidai mahakamani hapo kuwa, mshtakiwa alitenda kosa hilo Oktoba 9, 2014, saa 12 jioni katika eneo la Mji wa Zamani.

Alisema siku hiyo ya tukio mshtakiwa alikutana na mtoto huyo njiani akielekea nyumbani kwaondipo alipomshika mkonona kwenda naye kwenye pagala la nyumba katika mtaa huo.

Mwendesha mashtaka huyo aliieleza Mahakama hiyo kuwa, baada ya kuingia naye ndani mshtakiwa alitoa kisu na kuchoma kwenye ubao aliokuwa amemshikisha mtoto huyo ikiwa ni ishara ya kumtishia kisha alimwambia endapo atakataa kulawitiwa au akipiga kelele atamuua.

Sikwesa alidai baada ya vitisho hivyo ndipo mshtakiwa alipomvua nguo mtoto huyo na yeye suruali na kutoa sehemu zake za siri na kuupaka mate na kisha kuanza kumlawiti mtoto huyo kwa nguvu.

Alidai baada ya kumlawiti alimtishia kutotoa siri hiyo lakini mtoto huyo baada ya kufika kwa wazazi wake alilazimika kuwaambia kutokana na maumivu aliyokuwa nayo na ndipo walipotoa taarifa Polisi kabla ya kukamatwa.