RAIS KIKWETE ATEUA MAWAZIRI WAPYA

Rais Jakaya kikwete ametangaza mabadiliko katika baraza lake la mawaziri.

Rais amewateua mawaziri wanane wapya pamoja na manaibu watano.

Tangazo hilo lilifanywa na katibu katika ikulu ya rais balozi Ombeni Sefue.

Mabadiliko hayo yanajumuisha wadhfa wa waziri wa nishati na kawi wa Profesa Muhongo ambaye amejiuzulu mapema leo pamoja na wadhfa wa waziri wa ardhi ambao uliwachwa wazi baada ya kupigwa kalamu kwa Anna Tibaijuka.

Mawaziri hao wawili wanahusishwa na kashfa ya ufisadi ambayo ilimshinikiza mwanasheria mkuu pia kujiuzulu.

Rais Kikwete anatarajiwa kuwaapisha mawaziri hao wapya hii leo katika tangazo litakalorushwa hewani na runinga ya taifa.

Walioteuliwa

1. George Simbachawene- Waziri Nishati

2. Mary Nagu-Waziri wa Nchi mawasiliano na Uratibu

3. Christopher Chiza-Waziri uwezeshaji na Uwekezaji

4. Harson Mwakyembe-Ushirikiano wa afrika mashariki

5. Lukuvi-Ardhi Nyumba na Makazi

6. Steven Wasira-Kilimo chakula na Ushirika

7. Samwel Sitta -Wizara ya Uchukuzi

8. Jenista Muhagama-Sera na uratibu wa Bunge.