KIJANA APEWA URAIA KWA USHUJAA

Mwanamume mmoja mwenye asili ya nchini Mali ambaye aliwaficha wauza maduka katika duka kubwa maarufu kama supermarket mjini Paris wakati wa shambulio la kigaidi lililotekelezwa na watu wanaodhaniwa wapiganaji wa kiislamu amepewa hati halali ya ukaazi na kuwa raia halali wa Ufaransa.

Kwa pamoja waziri mkuu wa Ufaransa Manuel Valls na waziri wa mambo ya ndani Bernard Cazeneuve walizungumza katika karamu ya kumpongeza na kumshukuru Lassana Bathily kwa ushujaa wake kwa niaba ya taifa lake.

Kijana huyo ana umri wa miaka ishirini na minne, na kazi aifanyayo ni muuzaji msaidizi katika supermarket hiyo,ambaye alifanya kazi kubwa ya kuwaongoza na kuwaficha katika eneo la juu la chumba baridi cha kuhifadhia bidhaa na kisha akazima taa za duka hilo kubwa,kisha akawapigia polisi simu kwa msaada wakati walipovamiwa.

Baada ya tukio hilo, likapitishwa azimio aitwe apewe uraia wa nchihiyo ya Ufaransa ,hata hivyo inaelezwa kwamba Bathily ameishi nchini humo kwa miaka tisa sasa na alikuwa ameshaomba ridhaa ya kuwa raia halali wa nchi hiyo mwaka wa jana.

Wakati wa uvamizi huo, Amedy Coulibaly,aliwaua watu wane wenye asili ya Uyahudi katika duka hilo kubwa kabla hajapigwa risasi na polisi na kufa.