WANAJESHI 54 WAHUKUMIWA KIFO

Mahakama ya Nigeria imewahukumu kifo wanajeshi 54 kwa kukataa kupambana na wanamgambo wa Kiislamu wa Boko Haram.

Wanajeshi hao, walikutwa na hatia ya uasi, walishtakiwa kwa kukataa kuchukua miji mitatu ambayo ilikuwa imeshikiliwa na Boko Haram mwezi Agosti.

Mwanasheria wa wanajeshi hao alisema maafisa hao 54 watapigwa risasi.


Watano waliachiwa.

Vikosi vya kijeshi vililaumu kwamba havikuwa vimepewa silaha za kutosha na zana za kivita kupambana na Boko Haram.

Kundi hilo limekuwa likifanya mauaji tangu 2009 na linataka kuunda serikali ya Kiislamu kaskazini-mashariki mwa Nigeria.

Zaidi ya watu 2,000 wameshapoteza maisha katika mashambulizi hayo yanayodaiwa kufanywa na Boko Haram mpaka sasa na maelfu zaidi wamekosa makazi kutokana na mapigano hayo.