NDEGE YA AIR ASIA YAPOTEA NA WATU 160

Shirika la ndege la Air Asia linasema kuwa limeanzisha shughuli ya kuitafuta ndege yake iliyopoteza mawasiliano na kituo cha kuelekeza safari za ndege dakika 45 baada ya kuondoka kwenye mji wa Surabaya nchini Indonesia.

Zaidi ya watu 160 walikuwa ndani ya ndege hiyo ya Airbus 320 iliyokuwa safarini kwenda nchini Singapore.

Wengi wa abiria waliokuwa ndani ya ndege hiyo wanatoka nchini Indonesia.

Msemaji wa wizara ya usafiri nchini Indonesia amesema mawasiliano yalipotea kati ya visiwa vya Kalimantan na Java.

Wataalamu wa safari za ndege wanasema kuwa huenda ndege hiyo iliishiwa na mafuta