TALIBAN YAUA 100 SHULENI, WAKIWAMO WANAFUNZI 80

Takriban watu 100 wakiwemo wanafunzi 80 wameuwawa na wengine wengi kujeruhiwa baada ya wapiganaji wa Taliban kuvamia shule moja inayosimamiwa na jeshi huko Peshawar kaskazini - magharibi mwa Pakistan.

Wakuu wa Hospitali wanasema kuwa zaidi ya watu 40 wanasemekana kujeruhiwa japo idadi hiyo inatarajiwa kupanda zaidi.

Maafisa mjini Peshawar wanasema kuwa wanaume watano ama sita waliokuwa na silaha waliingia shuleni hapo wakiwa wamevalia magwanda ya kijeshi.

Wanafunzi mia tano na waalimu walikuwa katika shule hiyo ya umma ya kijeshi wakati sham,bulizi hilo lilipotokea.

Wakazi wa eneo hilop wanasema kuwa walisikia milio ya bunduki iliyodumu kwa dakika kadhaa.

Wanasema pia kuwa walisikia sauti za kelele za wanafunzi na waalimu.

Haijabainika wazi ni kwa namna gani wanamgambo wa Talebain waliweza kupenya hadi kuingia ndani ya majengo hayo yanayomilikiwa na jeshi.

Jeshi la Pakistan limesema operesheni ya uokozi ilikuwa ikiendelea na kwamba wengi wa wanafunzi na waalim wameokolewa toka eneo la hatari.

Shambulio hilo limetokea wakati operesheni kubwa ya kijeshi ikiendelea dhidi ya wapiganaji waTaleban wa Pakistan na wanamgambo wengine wanaoendesha harakati zao kaskazini mwa jimbo la Waziristan.