JOTO KALI KUATHIRI DAR, ZANZIBAR NA KILIMANJARO

HALI ya joto katika jiji la Dar es Salaam imeelezwa kupanda kwa nyuzi joto 4.5 kutoka 31.5 hadi 35.5 ambapo hali hiyo inatarajiwa kudumu hadi Februari mwakani.

Hayo yameelezwa na Mkurugenzi wa Huduma za Hali ya Hewa nchiniwa Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), Hamza Kabelwa ambapo alisema maeneo mengineambayo joto limepanda ni pamoja na Zanzibar na Kilimanjaro.

"Zanzibar joto limefikia nyuzi joto 34.4 kutoka 30.7 na Kilimanjaro ni 35.6 kutoka 31.6 na hali hii inaweza kuendelea katika vipindi tofauti hadi Februari mwakani," alisema.

Alisema hali hiyo inasababishwa naupepo unaotoka nchini Somalia kuja katika maeneo ya Nyanda za Juu Kusini, ambapo alifafanua kuwa kunatokana na kuwepo kwa kiwango cha juu cha joto katika baadhi ya maeneo.

Aidha alitumia nafasi hiyo kuwaondoa hofu wananchi kuwa mifumo ya upepo imebadilika kutokana na kuwepo kwa hali ya mvua katika ukanda huo.

"Mara nyingi ikifika Desemba, Januari na Februari huwa kunakuwa na joto kali katika maeneo ya Kaskazini mwa nchi na ukanda wa ziwa, kutokana na maeneo haya kuwa na misimu miwili ya mvua kwa mwaka,"alisema Kabelwa.

"Lakini hali hii hutokea kila baada ya miezi hiyo, ila wananchi wanasahau, cha msingi na wasisitiziwe kuwa wasiwena wasiwasi, hali hii itakwisha, na mwezi huu kutakuwa na mvua kwa vipindi tofauti," aliongeza.

Hata hivyo Kabelwa alisema TMA itakuwa ikitoa taarifa ya mabadiliko ya hali ya hewa kila wiki kuanzia sasa.