MBWEMBWE WAKATI WA KUMPOSA MPENZI WAKE ZAMTOKEA PUANI

Mwanamume mmoja raia wa udachi amejikuta akikimbilia usalama wake baada ya jaribio la kutaka kumposa mpenzi wake kwa mbwembwe kwenda mrama.

Mtu huyo ambaye hakutajwa kwa jina anayeishi mjini Ijsselstein alikodisha 'kreni' au Crane na kuipanda akipanga kwamba kreni hilo imtoe chini na kumpandisha hadi dirishani mwa mpenzi wake ambapo angemchezea wimbo na kisha kumposa.

Badala yake yaliyomkuta hakuyatarajia kabisa.

Kreni hiyo ilianguka chini na kupita dirishani kwa mpenzi wake huku ikiangukia nyumba za majirani.

Mwanamume huyo alilazimika kukimbilia usalama wake na hakuna aliyejeruhiwa katika tukiohilo lililowaacha wengi wakiangua kicheko.

Kwa mujibu wa jarida la Algemeen Dagblad, mpenzi wake mwanamume huyo alimkubali nakusema yuko radhi kuolewa naye licha ya tukio hilo.

Baada ya kuongea na polisi, wawili hao walisafiri kwenda mjini Paris Ufaransa kusherehekea.

Kreni hio ilianguka tena kwa mara ya pili ilipokuwa inainuliwa na hata kuharibu zaidi nyumba zamajirani. Meya wa mji huo, amezomewa na wengi baada ya eneo hilo kusemekana kutokuwa salama.