MWANAMKE ACHINJWA NA KUTENGANISHWA KICHWA

MKAZI wa kijiji cha Ilalangulu, kata ya Kibaoni wilayani Mlele, ElizabethRichard (16) ameuawa kwa kuchinjwa shingo, kichwa kikitenganishwa na kiwiliwili chake na watu wasiofahamika kisha wakanyofoa sehemu zake za siri na kuondoka nazo.

Aidha watu hao wamemkata mikono yake na titi lake la kushoto kwa kitu chenye ncha kali.

Kamandawa Polisi mkoa wa Katavi, Dhahiri Kidavashari alibainisha kuwa mikono ya Elizabeth na titi lake la kushoto vilifukiwa ardhini karibu na ulikofukiwa mwili wake.

Kidavashari aliongeza kuwa chanzo cha mauaji hayo yaliyotokea juzi, saa 4:00 asubuhi kijijini Ilalangulu inaonekana ni imani za kishirikina.

Kwa upande wake mume wa marehemu, Hevinie Kagembe (45) alidai kuwa asubuhi ya siku hiyo ya tukio aliongozana na mkewe kwenda shambani eneo la Kazarohokulima.

"Mimi na mke wangu kila mmoja wetu ana shamba lake na yako maeneo tofauti," alidai Kagembe. Inadaiwa ilipotimu saa kumi mchana mume wa marehemu alirejea nyumbani kijijini humo lakini hakumkuta mkewe.

"Kawaida ya wanandoa hao , mke alikuwa akirudi nyumbani mapema na kuandaa chakula lakini siku hiyo haikuwa hivyo ... ilipotimu saa mbiliusiku marehemu alikuwa bado hajarejea nyumbani ... mume wa marehemu aliingiwa na mashaka hata alipompigia simu mama mzazi wa marehemu alijibiwa kuwa siku hiyo marehemu hakuwahi kufika nyumbani kwake, " alieleza Kamanda Kidavashari.

Inadaiwa siku iliyofuata saa mbili asubuhi mkazi wa kijijini humo ambaye alikuwa akipita shambani kwa marehemu akielekea shambanikwake kulima aligutuka kuona kifusicha udongo kikiashiria kufukiwa kwakitu ardhini.

Akizungumzia mkasa huyo , shuhuda huyo alieleza kuwa baada ya kuona kifusi hicho cha udongo alichukua kijiti na kuanza kufukua ghafla akaona nywele na hereni ambapo alikimbia kurudi kijijini na kutaarifu uongozi ambao ulilitaarifuJeshi la Polisi.

Kwa mujibu wa Kamanda Kidavashari askari Polisi walipofika eneo la tukio waliufukua mwili wa marehemu kichwa kikiwa kimetenganishwa na kiwili chake lakini haukuwa na mikono wala titi la kushoto pia nyeti zake zilikuwa zimenyofolewa.

"Ndipo walipoona dalili ya kufukiwa kitu karibu na ulipofukiwa mwili wa marehemu walipofukua walikuta mikono ya marehemu na titi lake lakushoto vikiwa vimefukiwa," alibainisha Kidavashari.

Kamanda Kidavashari alidai kuwa Jeshi la Polisi linaendesha msako katika maeneo mbalimbali wilayani ili kuwakamata wote waliohusika na mauaji hayo ili sheria iweze kuchukua mkondo wake.

Chanzo: Habari Leo