MPANDA DC WAMALIZA UJENZI WA MAABARA

HALMASHAURI ya Mpanda katika Mkoa wa Katavi imetekeleza agizo la Rais Jakaya Kikwete kwa kukamilisha ujenzi wa vyumba vyote 17 vya maabara kwa ajili ya masomo ya sayansi katika shule sita za sekondari wilayani humo, ujenzi uliogharimu zaidi ya Sh milioni 568.6.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mpanda, Estomihn Chang'ah alimweleza Mkuu wa Wilaya ya Mpanda, Paza Mwamlima kuwa utekelezaji wake umefikia asilimia 90 ambapo kazi iliyobaki ni kuweka vifaa vya maabara tu katika majengo hayo.

Alieleza kuwa ujenzi wa maabara hizo ulianza Januari 14 mwaka huu na kwamba zaidi ya Sh milioni 688.3 zilitengwa kwa ajili ya ujenzi huo wa maabara. Hata hivyo zaidi ya Sh milioni 568.6 zimetumika.

Alizitaja shule hizo ambazo zimekamilisha ujenzi wa majengo ya maabara hizo kuwa ni pamoja na Mwese, Karema, Ikola, Mpandandogo, Ilandamilumba na Kabungu.


Chanzo: Habari leo