MWANAMKE MMOJA AMTUPA MJUKUU WAKE DIRISHANI WAKATI BASI LIKIWA KWENYE MWENDO

Katika hali isiyo kuwa ya kawaida mama moja aliye kuwa akisafiri na mtoto wake mmoja na wajukuu zake wawili, aliamua kumtupa mjukuu wake wa miaka sita dirishani huku basi likiwa katika mwendo kasi na kusababisha kifo chake baada ya kufikishwa katika hospitali ya mkoa wa Singida.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo kamanda wa jeshi la polisi mkoani Singida ACP Thobias Sedoyeka, amesema mama huyo aliye tambulika kwa jina la Lawaridi Saidi mweye umri wa miaka 46 aliyekuwa akisafiri na basi namba T 981 ALS kampuni ya Salumu Clasc lilokuwa likitokea Dar-es-salaam na kuelekea Kigoma.

Amesema alipofika katika kijiji cha Iguguno wilaya ya Mkalama siku ya tarehe 18/12/2014 saa 2 usiku alimtupa mjukuu wake Mayasa meshaki dirisani huku basi likiwa katika mwendo kasi.

Kwa upande wake mganga wa zamu katika hospitali ya mkoa wa Singida Dkt Adamu Hussein amesema walimpokea mtoto huyo akiwa katika hali mbaya akiwa hapumui vizuri na damu kutoka katika masikio, baada ya kumpatia matibabu alilazwa na siku ya pili alifariki kutokana na kupasuka kwa fuvu la kichwa.

Akieleza jinsi alivyo mtupa mjukuu wake huku basi likiwa katika mwendo kasi Lawaridi Saidi ambaye ni mkazi wa Kongowe jijini Dar-es-salaam amesema baada ya kuamka akiwa katika hali ya usingizi alijikuta akimchukuwa mjukuu wakeMayasa na kumtupa dirishani na hatimaye abiria wakaanza kumpiga na kuamuru basi lisimame na kumtafuta mtoto huyo.