BODABODA AUAWA KWA KUCHOMWA KISU

Mwendesha pikipiki(BODABODA) aliyejulikana kwa jina la Zakaria Lungwa(24) mkazi wa Mtaa wa Kawajense Madukani Wilayani Mpanda Mkoani hapa ameuwawa kikatili kwa kuchomwa na vifu tumboni na watu wawili ambao alikuwa akiwafafamu kwa sura na kupolwa pikipiki yake.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alisema mauwaji ya kikatili ya Bodaboda huyo yalitokea hapo majira ya saa saba na robo usiku katika mtaa wa Nsemulwa Kichangani mjini Mpanda Alisema siku hiyo ya tukio marehemu alikuwa na pikipiki yake aina ya Sanya yenye rangi nyekundu yenye namba za usajiri T.752 CQS akiwa huko kwenye maeneo ya Night Club iliyoko mtaa wa Madini akiwa kwenye shughuli zake za kila siku Akiwa kwenye eneo hilo la Night Club marehemu alipata mteja mmoja wa kiume ambae alimbeba kwenye pikipiki yake na kuelekea Mtaa wa Nsemulwa Kichangani

Kamanda Kidavashari alieleza walipofika katika eneo la Mtaa wa Nsemulwa Kichangani mteja yule aliyempakia alimuamuru marehemu asimame katika eneo ambalo hata alikuwa na nyumba yoyote hapo.

Ghafla katika eneo hilo alitokea mtu mwingine mwanaume na alianza kumwambia marehemu ashuke kwenye pikipiki yake na kisha alimvuta chini pembeni ya barabara.

Alisema baada ya kuona hari hiyo marehemu alipiga mayowe ya kuomba msaada kwa majirani wa eneo hilo hata hivyo hakuweza kupata msaada wowote kutoka kwa majirani wanaoishi kwenye eneo hilo

Mmoja kati ya watu wale wawili alitoa kisu na kisha alimchoma marehemu tumboni na kisha marehemu alianguka chini na watu hao walichukua pikipiki na kisha walitokomea kusiko julikana huku wakiwa wamemuacha marehemu akiwa anagalagala chini akiwa anatokwa na damu.

Kamanda Kidavashari alisema marehemu alipata msaada wa kupelekwa hospitali ya Wilaya ya Mpanda baada ya mtu mmoja aliyekuwa akipita kwenye eneo hilo akiwa na gari lake alipomwona marehemu akiwa anagalagala pembeni ya barabara.

Alisema marehemu baada ya kufikishwa katika Hospitali ya Wilaya ya Mpanda alianza kupatiwa matibabu na wakati akiwa anaendelea kupatiwa matibabu ambapo ilipofikia majira ya saa kumi na mbili jioni alifariki Dunia

Kidavashari alieleza Jeshi la Polisi linamshikilia mtu mmoja anaejulikana kwa jina la Khalid Seif (24) Mkazi wa Mtaa wa Nsemulwa kuhusiana na tukio hilo ambae anadaiwa kuwa alionekana katika eneo hilo la Night Club akiwa na mteja aliyeondoka na marehemu

Alisema hata hivyo jeshi la polisi linaendelea na upelelezi ilikubaini watuhumiwa waliohusika na mauwaji hayo ya kikatili

Kamanda Kidavashari ametowa wito kwa madreva wote wa Bodaboda wa Mkoa wa Katavi wanapo ona kumekuwa usiku kama wamepata mteja basi wawe wanakuwa madreva wawili wanaongozana ilikuweza kusaidiana kama kutatokea tatizo lolote.

Chanzo:Katavi yetu