ALIYOTOROSHA TWIGA JELA MIAKA 60

HATIMAYE Mahakamaya hakimu mkazi Moshi, mkoani Kilimanjaro, imemhukumu miaka 60 jela, Kamran Ahmed, raia wa Pakistani kwa kosa la kutorosha wanyama hai 153, wakiwemo Twiga wanne Hata hivyo mtuhumiwa huyo mpaka sasa haijulikani alipokimbilia baada ya kutoweka hapa nchini tangu mwanzoni mwa mwaka huu.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu mkazi mfawidhi ,Simoni Kobelo, alisema Mahakama hiyo imewaachia huru Watanzania watatu baada ya kutokuwapo kwa ushahidi wa kuwatia hatiani.

Kobelo, alisema Mahakama imeridhishwa na ushahidi uliotolewa na dhidi ya mtuhumiwa huyo na kumtia hatiani kwa makosa yote manne yaliyowasilishwa na Jamhuri Kobelo alisema Mahakama imewaachia huru Watanzania watatu ambao ni Hawa Mang'unyuka, Mathew Kimathi na Michael Odisha Mrutu kwa sababu ya Jamhuri kushindwa kuthibitisha ushahidi stahiki.

Alisema ushahidi uliowasilishwa haukuonesha kuwaunganisha washitakiwa hao moja kwa moja na kosa la kusafirisha wanyama hai nje ya nchi.

Katika hukumu hiyo, Kamran, alikutwa na makosa manne, kushiriki na kula njama ya kutenda uhalifu kinyume cha kifungu 57 (1), sehemu ya 4(1), sura ya kwanza ya kosa la uhujumu uchumi na kushiriki utoroshaji wa wanyama hai wenye thamani ya shilingi milioni 170.5

Kosa la pili ni kufanyabiashara ya kukamatana kusafirisha wanyama hai wakiwemo Twiga, Chui, Pofu, Punda Milia, Swala ndege wa aina mbalimbali, Duma, Nyati bila leseni.

Kosa la tatu ni kukutwa na Nyara za Serikali katika uwanjawa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA), Novemba 26, mwaka 2010 na kosa la nne ni la kuisababishia serikali hasara ya Dola 113.7 kwa kufanya biashara kinyume cha sheria.

Kuhusu mshitkakiwa wa pili Hawa Mang'unyuka anayetajwa kuwa mmiliki wa kampuni ya Harm Marketing na Luwego Bird Trappers, inayodaiwa leseni yake kutumika kuhalalisha ukamatajina utoroshaji huo, Hakimu Kobelo alisema kwa mujibu wa vielelezo vilivyowasilishwa kampuni ya Hawa, ilipewa kibali halali cha kukamata wanyama hai na mamlaka husika Washitakiwa Mathew Kimathi na Michael Mrutu, Kobelo alisema kwa sababu hakuna sehemu yoyote inayoonesha ushiriki wao katika utoroshaji zaidi kutekeleza wajibu wao kama walivyoekezwa na wakuu wao wa kazi kipindi hicho.

Machi mwaka huu Mahakama ya HakimuMkazi, ilitoa amri ya kukamatwa ndani ya saa 24, mshitakiwa namba moja(Kamran)baada yakushindwa kuhudhuria mahakamani hapo kwa zaidi ya vikao viwili mfululizo.

Amri ya kukamatwa kwa raia huyo wa Pakstani ilitolewa Machi 23 mwaka huu Hakimu Kobelo baadaya kutoa hati ya kukamatwa kwa raia huyo kufuatia ombi lamawakili wa upande wa Jamhuri kuomba hati hiyo kutolewa kutokana mshitakiwa kutofika mahakamani.

Kutoroka kwa mtuhumiwa huyo kuliilazimu Mahakama kutoa hati ya hati ya kukamatwa (Arrest warrant) kwa wadhamini wawili wa mshitakiwa huyo ambaye ilidaiwa tayari ametorokea nje ya nchi.

Wadhamini waliotajwa mahakamani hapo , Jackson Kimambo na Peter Temba,ambao awali walipewa wito wa kufika mahakamani hapo kutoa uthibitisho wa uwepo wao ikiwa ni pamoja na kusaidia mahakama kumpata mshitakiwa huyo kama walivyosaini katika hati yao ya udhamini.

Hata hivyo Mdhamini mmoja Peter Temba ndiye alikamatwa na kuhukumiwa kifungo jela na Jackson Kimambo hakukamatwa.

Kesi hiyo iliyokuwa na mvuto wa kitaifa na kimataifa, Novemba 25 mwaka 2010 watuhumiwa hao wanadaiwa kula njama ya kusafirisha nje ya nchi zaidi ya wanyama hai na ndege 100 wakiwemo Twiga wanne ambao thamani yake inakadiliwa kufikia dola za marekani 113,715.

Kamran amebainika kutenda kosa la kusafirisha wanyama hai kwenda Doha, nchini Oman kwa kutumia ndege aina ya C.17 yenye nambari AMA/MAB mali ya shirika la Qatar Airways.

Kwa mujibu wa hati ya mashitaka ni kwamba wanyama hao, walisafirisha kwenda Falme za Kiarabu baada ya kupita vizuizi yakiwamo mageti ya namba 5A na 5B katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA).

Chanzo: Tanzania Daima