KAMBI YA AU SOMALIA YAVAMIWA NA AL-SHABAAB

Jeshi la kulinda amani la Umoja wa Afrika nchini Somalia limesema askari wake watatu na kandarasi raia wameuawa katika shambulio lililofanyika katika makao yake makuu mjini Mogadishu.

Taarifa ya Umoja wa Afrika imesema wapiganaji wa al-Shabab waliingia katika kambi wakivalia sare kama askari wa jeshi la serikali ya Somalia.

Taarifa hiyo imesema washambuliaji watano waliuawa na wengine kadha kukamatwa.

Pamoja na kutoa eneo hilo kuwa makao makuu ya majeshi ya kulinda amani ya AU nchini Somalia, eneo hilo lililoimarishwa pia makao ya balozi za Uingereza na Italia.