BARCELONA WAFUNGIWA KUSAJILI MPAKA 2016

Shirikisho la soka dunia FIFA limeitupilia mbali rufaa iliyokatwa na klabu ya Barcelona kuhusu kuizuia kusajili kwa kukiuka kanuni ya usajili.

Barca walifungiwa kwa miezi 14 kusajili baada ya kufanya makosa kwa kusajili kinda wa chini ya miaka 18, Ikiwa ni kinyume na kanuni za usajili za Fifa.

Kwa maamuzi haya timu hii haitakua na uwezo wa kusajili mchezaji mpya mpaka Januari 2016.

Barcelona wanatarajia kukata rufaa tena maamuzi haya ya Fifa kwenye mahakama ya usuhuhishimichezoni(Cas).

Miamba hiyo ya soka ilifanikiwa kuwasajili mshambuliaji Luis Suarez , mabeki Thomas Vermaelen Jeremy Mathieu golikipa Claudio Bravo na kiungo Ivan Rakitic mwanzoni mwa msimu baada ya baada ya kupewa ruhusa maalumu na Fifa.