RAIS KIKWETE AMTEUA MWANASHERIA MKUU MPYA

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dr. Jakaya Mrisho Kikwete amemteua Profesa Justice Ibrahim Juma kuwa mwanasheria mkuu wa serikali (AG).

Uteuzi huo umefuatia baada yaaliyekuwa mwanasheria mkuu Frederick Werema kutangaza kujiuzulu kutokana na skandali ya mabilioni ya akaunti ya Escrow.

Mapema mwezi huu Rais Jakaya Kikwete pia alimteua Profesa Juma Assad (CAG) kuwamkaguzi na mdhibiti wa hesabuza serikali baada ya Ludovick Utouh kumaliza muda wake.