WATU 60 WANUSURIKA KIFO

Watu zaidi ya 60 waliokuwa wakisafiri wamenusurika kifo huku wengine wakijeruhiwa baada ya basi la Mtei Express Coach kuyagonga magari matatu katika eneo la kijiji cha Mawemairo Wilayani Babati Mkoani Manyara kilichopo katika barabara kuu inayotoka mjini babati kuelekea mkoani Arusha.

Ajali hiyo imelihusisha bus hilo lenye namba za usajili T 729 bes wakati lilipokuwa likitokea mjini Babati kuelekea mkoani Arusha na kwa mujibu wa mashuhuda waliokuwa wakisafiri wamesema lilipofika katika eneo hilo,dereva wa basi hilo alishindishwa kulimudu wakati alipopewa ishara na wafanyakazi wa kampuni ya ujenzi wa barabara ya serikali ya china(Chico) kusubiri lori lililokuwa likishusha matofali kwa ajili ya ukarabati wa karavati na hatimaye kuyagonga magari yaliyokuwa yakisubiri lori hilo.


Nae mganga mfawidhi katika hospitali ya Halmashauri ya mji wa Babati Bw Mosses Mollel amesema amepokea majeruhi wanane na mpaka sasa amebaki majeruhi mmoja huku wengine wamepata ruksa baada ya kupatiwa matibabu.

Chanzo:ITV