MADIWANI WAGOMA KUJADILI TAARIFA YA KAMATI YA FEDHA

Mpanda Katavi

Madiwani wa Halimashauri ya Mji wa Mpanda Mkoa wa Katavi wamekataa kujadili taarifa ya kamati ya fedha na mipango ya Halmashauri hiyo iliyo wasilishwa kwenye kakao cha Baraza la madiwani kilichofanyika juzi kwenye ukumbi wa Chuo Kikuu Huria cha Mkoa wa Katavi.

Baraza hilo la madiwani lilikataa kupitisha taarifa hiyo kufuatia hoja mbalimbali zilizotolewa na Madiwani ambao walidai kuwa taarifa hiyo iliyoletwa mbele ya kikao hicho haikuwa imejitosheleza.

Miongoni mwa kasoro zilizodaiwa kuwemo kwenye taarifa hiyo ni kutokuwemo kwa viambata vinavyo onyesha namna ya mapato yandani yalivyo kusanywa na sehemu yaliko tokaDiwani wa kwanza kipinga taarifa hiyo kwenye kikao hicho cha Baraza la madiwani kilicho kuwa kinaongozwa na makamu mwenyekiti wa Halimashauri ya mji wa Mpanda Yusuph Ngasa.

Alikuwa ni Diwani wa Kata ya Shanwe Abel Kapini Diwani Kapini alidai kuwa taarifa hiyo inamapungufu ambayo yatawafanya madiwani kama wataamua kuijadili washindwe kuijadili kitaalamu kwani haina mchanganuo ambao utawawezesha madiwani kuhoji taarifa hiyo ya kamatiya fedha na mipango Kwa upande wake diwani wa Kata ya Ilembo Wensilaus Kaputa alilieleza Baraza hilo kuwa taarifa hiyo haiko wazi kwani inaonekana taarifa zake zimefichwa kwa hari hiyo ni vizuri irudishwe ikaandaliwe upya.

Mwenyekiti wa kikao cha baraza la madiwani baada ya kutolewa hoja hizo aliwashauri madiwani wapige kura ili kujua ni madiwani wangapi wanao unga mkono hoja hiyo ya kuikataa taarifa hiyo.

Kufuatia uamuzi wa mwenyekiti madiwani walipiga kura ambapo kulikuwa na madiwani kumi kwenye kikao hicho na madiwani wanane waliunga mkono kuikataa taarifa hiyo na madiwani wawili waliikubali Nae Mkugenzi wa Halimashauri ya Mji wa Mpanda Selamani Lukanga alihaidi kuwa kikao kijacho cha Baraza hilo watasomewa taarifa ikiwa na viambatanisho na mchanganuo kama ambavyo walivyo hitaji madiwani.


Source:Katavi Yetu