MAMA YAKE UFOO SARO ALIPIGWA RISASI TANO

TAARIFA zaidi za kusikitisha kuhusumauaji ya kinyama, yaliyofanyika katika familia ya Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha ITV, UfooSaro zimeendelea kutolewa, ambapo imebainika mama mzazi wa mtangazaji huyo, Anastazia Saro(58), aliuawa kwa kupigwa risasi tano.

Msemaji wa familia hiyo, Idd Lemaalisema hayo jana wakati wa ibada ya kumuaga Anastazia, iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa Kibwegere, Dar es Salaam.

Awali, taarifa zilizokuwepo, zilidai Anastazia alipigwa risasi mbili kifuani, lakini Lema alisema baada ya uchunguzi wa mwili huo uliofanywa na Polisi, ilibainika kuwa alipigwa risasi tano na si mbili.

Akizungumza wakati wa ibada ya kumuaga Anastazia, ambayo mwanawe wa pekee Ufoo hakuweza kuhudhuria, Mwinjilisti wa Kanisa hilo, Margaret Shekoloa alisema Anastazia atakumbukwa kwa mambo mengi, aliyoyafanya katika Kanisa hilo katika nafasi mbalimbali alizokuwa nazo ukiachaya muumini.

Alisema siku moja kabla ya kifo chake, Anastazia alikwenda kanisani na kupanda maua katika bustani ya kanisa na kupamba madhabahu.

"Alipomaliza kupamba madhabau pamoja na kupanda maua katika bustani, aliniaga na kuniambia mchungaji tutaonana katika ibada ya kesho bila kujua kuwa siku hiyo hataiona," alisema Mwinjilisti Shekoloa.

Alisema matukio ya ukatili, kwa sasa yamezidi kuongezeka nchini na chanzo chake ni watu kutokuwa karibu na Mungu wao. Alisema matukio hayo, yanayowagusa watu wengi wasio na hatia, pia yamekuwa yakichangia uvunjifu waamani.

"Anastazia alikuwa na malengo makubwa na Kanisa hili, aliwaunganisha wanawake wote kwa kuwapa mafunzo ya ujasiriamali," alisema Shekoloa.

Alisema hata pale alipohitajika na kanisa kwa ajili ya kutoa mafunzo ya ujasiriamali kwa vijana, aliitikia mwito bila tatizo lolote.

Ibada ya kuaga mwili huo ilimalizika saa 11.30 jioni na mwili huo kusafirishwa kwenda kijiji cha Shali, Machame mkoani Kilimanjaro.