HUKUMU YA BABU SEYA NA PAPII KOCHA YAANZA KUSIKILIZWA MAHAKAMA YA RUFAA

Hukumu ya Nguza Viking maarufu kama babu Seya imeanza kupitiwa.

Mahakama ya rufaa imeanza kupitia hukumu ya mwanamuziki maarufu nchini mwenye asili ya jamhuri ya kidemokrasia ya congo DRC Nguza Viking maarufu kama Babu seya na mwanawe Johnson Nguza maarufu kama Papii kocha.

Mapitio hayo yanafanywa na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Mh Nathali Kimaro amboa ndio waliotoa hukumu Februari 2010 kwa upande wa waleta maombi wakiongozwa na wakili Mabetre Marando wamewasilisha mahakamani hapo mambo sita ambayo wangepedwa mahakama hiyo iyaangaliye kwa makini,ambapo moja ya mambo hayo ni pamoja na kuwa wakati wa usikilizwaji wa kesi mashahidu muhimu hawakuitwa kutoa ushaidi wao.


Aidha wanataka ushaidi wa watoto uliotolewe katika kesi hiyo uondolewe katika kumbukumbu kwa sababu haukufuta taratibu na vigezo vya matwakwa ya sheria ya ushaidi pia wamesema kuwa katika ushaidi uliotolewa ulionyesha kuwa katika nyumba ya babu seya kulikuwa na mlango wa siri lakini mahakama ilipokwenda hapo mlango huo haukuonekana.

Kwa upande wa serikali kupitia wakili wake mwandamizi jackson burashi wameiomba mahakma hiyo kutupilia mbali shauri hilo kutokana na ukweli kuwa yapo hapo kinyume na sheria na yameletwa kama rufaa na siyo mapitio.


Aidha akaongeza kuwa maombi hayo hayajakidhi viwango vya sababu za mapitio kwa kuwa maombi hayo yalipaswa kuonyesha kuwa kosa limetendeka na haki ya mleta rufaa imepotea. Baada ya maelezo ya pande zote mbili mahakama ikasema itatoa maamuazi baada ya kupitia maelezo ya pande zote mbili.

Babu Seya na mwanaye papii kocha wanaendelea kutumikia kifungo cha maisha jela baada ya kukutwa na hati ya makosa ya kunajisi na kulawiti watoto wadogo kupitia huku iliyotolewa na mahakama ya hakimu mkazi kisutu mwaka 2004 ambapo walihkumiwa kifungo cha maisha.