DIWANI ACHEZEA KICHAPO HUKU MTU MMOJA AKIUWAWA KWA RISASI MKOANI KATAVI

Diwani wa Kata ya Majimoto Tarafa ya Mamba Wilaya ya Mlele Mkoa wa Katavi Nyasongwe (45) amejeruhiwa vibaya na kulazwa hospitalini baada ya kupigwa na askari wanaofanya oparesheni kimbunga katika Mkoa wa Katavi wakati akiwa msibani kwa mwanakijiji aliye uwawa kwa kupigwa risasi na Askari wanaofanya oparesheni kimbunga baadaya kutokea vurugu baina yao na wanakijiji cha Luchima kata ya Majimoto Wilaya ya Mlele mkoa wa Katavi.

Akiongea kwa taabu na waandishi wa habari Diwani huyo wa Kata ya Majimoto ambae amelazwa katika wodi namba moja huku akiwa chini ya ulinzi wa Polisi katika wodi namba moja katika hospitali ya wilaya ya Mpanda ambako amelazwa Alisema tukio hilo na kupigwa na kujeruhiwa lilitokea hapo oktoba 13 mwaka huu majira ya saa sita mchana wakati akiwa msibani kijijini hapo alipokuwa amekwenda kwenye msiba wa mwanakijiji ambae alikuwa ameuwa muda mfupi kwa kupigwa risasi na askari wanaofanya opuresheni Kimbunga.

Alieleza kuwa siku hiyo ya tukio yeye wakiwa na Afisa Tarafa wa Tarafa ya Mamba Lyoba Juma Shomari walipata taarifa kuwa kumetokea vurugu baina ya wanakijiji cha Luchima na Askari wanaofanya opuresheni Kimbunga na kusababisha kifo cha mwanakijiji mmoja na kushambuliwa na kujeruhiwa kwa mkuu wa kituo cha kutuliza ghasia wa Mkoa wa Katavi ASP Mafie Diwani huyo ambae ameumia vibaya sehemu yamatako.

Alisema ndipo walipokubaliana na afisa tarafa huyo na kuelekea kwenye eneo la tukio ambapo walikuta wanakijiji wakiwa wameweka tayari msiba wa mwanakijii mwenzao ambae alikuwa ameuwawa kwa kupigwa risasi Alifafanua kuwa kifo cha mwanajijiji huyo kilitokana na vurugu zilizotokana na wanakijiji hicho kutoridhishwa kuona mwenzao mmoja nyumba yake ikipekuliwa na kikosi cha opareshen kimbunga ndipo walipoamua kumshambulia kwa fimbo ASP Mafie na kujeruhi kichwani na kumfanya kupoteza fahamu.

Pia wanakijiji hao walilishambulia kwa mawe gari la polisi lenye namba PT 0985 na kulivunja kioo ndipo askari hao wa opuresheni kimbunga walipo amua kufyatua risasi ambayo ilimuuwa mwanakijiji huyo na kumjeruhi mguuni mwakakijiji mwingine ambae amepelekwa Katika hospitali ya Sumbawanga mkoani Rukwa kwa ajiri ya matibabu Serengeti alieleza kuwa wakati wakiwa bado wako hapo msibani ghafla lilitokea kundi la askari wa opuresheni kimbunga na kuanza kuwashambulia waombolezaji wote waliokuwepo hapo bila kujali jinsia ingawa yeye na afisa Tarafa hiyo waliweza kujitambulisha lakini waliendelea kupokea kipigo bila huruma kutoka kwa askari hao.

Alieleza kuwa kisha walipakiwa kwenye roli la jeshi wakiwa na kundi la watu waliokuwa wanaomboleza msibani hapo kwa kudaiwa kumshambulia mkuu wa kikosi cha kutuliza ghasia wa Mkoa wa Katavi.

Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Katavi Dhahiri Kidavashari alipotakiwa kutowa ufafanuzi kuhusiana na tukio hili alisema kuwa opuresheni hiyo Kimbunga mhusika ambae anatakiwa kutowa taarifa za tukio hili ni mkuu wa Hifadhi ya wanyama pori ya Katavi Kwa upande wake mkuu wa Hifadhi ya Katavi Ignasi Gara alishindwa kutowa kabisa ushirikiano kwa waandishi wa habari na kuatupia jeshi la wananchi kuwa wao ndio wasemaji wakuu.


Chanzo:Katavi Yetu blog