MUHONGO AAGIZA HALMASHAURI KUTOA TAARIFA ZA USHURU WA MADINI

Waziri wa Nishati na Madini Profesa Sospeter Muhongo amezitaka Halmashauri zote Nchini ambazo maeneo yao yana migodi ya madini kuhakikisha wanatowa taarifa za fedha zinazopatikana kutokana na ushuru wa madini kwa wananchi wao.

Waziri Muhongo alitowa kauli hiyo wakati akiwahutubia viongozi wa Mkoawa Katavi na wachimbaji wa madini katika mkutano uliofanyika kwenye ukumbi Wa Idara ya maji wa Halmashauri ya Wilaya ya Mpanda wakati wa ziara yake ya siku mbili ya kukagua miradi ya maendeleo ya Wizara hiyo.

Alieleza kuwa wananchi katika maeneo mbalimbali hapa nchini wamekuwa wakipotosha kuwa Halmashauri zimekuwa hazipatiushuru kwenye maeneo yao unaotokana na ushuru unaotokana na madini kitu ambacho sio sahihi Alisema hakikisheni mnawasomea wananchi wenu mapato yote ambayo Halmashauri zenu zinapata kutoka kwenye makampuni yanayochimba madini badala ya kuwaficha wananchi na matokeo yake yamekuwa ni wananchi kujenga chuki kwa makampuni hayo wakijua kuwa Halmashauri zao hazipati chochote kutoka kwa makampuni ya uchimbaji wa madini Pia alizitaka Halmashauri kuhakikisha fedha wanazolipwa kutokana na ushuru wa madini zinatumika kwa ajiri ya shughuli za maendeleo kwenye maeneo yote.

Profesa Muhongo alieleza zipo baadhi ya Halshauri wamekuwa wakitumia pesa hizo kwa ajili ya watumishi wao kwenda kujifundisha namna ya kuzowa taka kwenye mikoa mingine hayo siyo matumizi mazuri ya fedha alisema Muhongo Aidha alieleza kuwa serikali imeshaweka utaratibu ambao hakuna mgodi ambao unaanzishwa hapa Nchini bila kuwa na ubia na Serikali ndio utaratibu ambao umeisha wekwa na wizara hiyo kwani kama tulikosea mwanzo hatutakiwi kukosea tena Pia aliwashauri wachimbaji wadogo wadogo waanzishe vyama vyao ili iwe rahisi kwao kukopeshwa mikopo ambayo itawasaidia kununua vifaa vya kisasa.

Viongozi wa wachimbaji wawe na utaratibu wa kuwasikiliza kero za wachimbaji vijijini kuliko ilivyo sasa ambapo wachimbaji wanapiga simu mojakwa moja kwa waziri Kwa upande wake Mkuu wa Mkoa wa Katavi DR Rajabu Rutengwe alieleza kuwa mbali ya mkoa kuwa na madini mbalimbali kama vile Dhahabu Shaba bado wachimbaji wanakabiliwa na changamoto mbalimbali Rutengwe alizitaja baadhi ya changamoto hizo kuwani vifaa duni wanavyotumia kuchimbia na mitaji midogo kwa wachimbaji.

Nae Mwenyekiti wa wachimbaji wadogo wa Mkoa wa Katavi Willy Mbogo alimweleza waziri Muhogo kuwa jumla ya leseni 1035 zimeisha tolewa kwa wachimbaji wadogo wa Mkoa wa Katavi.


Source: Katavi yetu