MASHABIKI WA DORTMUND WAVUNJA VITI EMIRATES

Kama ulizani tatizo lipo kwa watanzania tu kung'oa viti uwanja wa taifa basi ondoa mawazo hayo.

Mashabiki wa Borussia Dortmund kutoka Ujerumani wamevunja na kung'oa viti(Pichani) katika uwanja wa Emirates unaomilikiwa na klabu ya Arsenal kutoka Uingereza.

Tukio lilitokea siku ya jumanne wakati timu hizo zilipokutana katika mchuano wa ligi ya klabu bingwa ulaya ambapo Dortmund waliondoka na ushindi wa goli 2 kwa 1.

Magoli katika mchezo huo yalifungwa na H. Mkhitaryan wa Borussia Dortmund katika dakika ya 18 ya michezo kabla ya mfungaji wa Arsenal Olivier Giroud kusawazisha katika dakika ya 45 ya kipindi cha kwanza.

Alikuwa ni Roberto Lewandowski aliyepigilia msumari wa mwisho katika dakika ya 85 na kufanya ubao wa matangazo kusomeka Arsenal 1-2 B. Dortmund na kuharibu furaha ya kocha Arsene Wenger ambae ilikuwa siku yake ya kuzaliwa na kufikisha miaka 64.

Arsenal bado wanashikilia usukani wa kundi huku wakiwa pointi sawa na Dortmund pointi 6 tofauti ya magoli imeibeba Arsenal. Baada ya Dortmund wanafuata Napol kutoka Italy wakiwa na pointi 6 kisha Marseille ya Ufaransa ikiwa haina kitu.