KATI YA VIJANA 10, 6 WANAPIGA PICHA AU VIDEO YA NGONO NA KUISAMBAZA

Sita kati ya vijana 10 wanasema kuwa wameombwa picha au video za kingono. Hii ni kwa mujibu wa utafiti a kitengo kuhusu maslahi ya watoto Uingereza ambao BBC iliweza kuuona

Kati ya waliohojiwa , asilimia arobaini walisema kuwa walijipiga picha au kunasa video wakiwa katika vitendo vya ngono na karibu robo yao walimtumia mtu picha hizo kwanjia ya SMS au ujumbe mfupi.

Mkuu wa kitengo hicho, Peter Wanless, alisema kuwa "sexting" au jambo la vijana kutuma ujumbe wenye mada ya ngono limekuwa la kawaida miongoni mwa vijana Uingereza.

Matokoe haya yanaonyesha kuwa tabia hii inafanyika sana miongoni mwa vijana na ni moja ya mambo ambayo vijana hufanya katika mahusiano yao.

Katika utafiti huu vijana 450 walihojiwa kuhusu tabia hiyo kote nchini.

Miongoni mwa wale waliohojiwa kuhusu kutuma picha zao za ngono au video kwa njia ya simu asilimia hamsini walisema kuwa waliituma picha hiyo kwa wapenzi wao wanaume au marafiki zao wa kike, lakini thuluthi moja wakasema kuwa walimtumia mtu wasiyemjua kwenye mtandao wa internet.

Lakini wataalamu wanasema kuwa watu wanawadhalilisha vijana kwa kuwataka wawatumie picha zao kwa kutumia vitisho.

Miongoni mwa wale waliosema kuwa walimtumia mtu picha yao, , asilimia 20 walisema kuwa waligundua watu walichangia picha zao wakati wengine wakisema hawajui zilikokwenda picha zao.

Kulingana na sheria za Uingereza ni halali kujihusisha na ngono ukiwa na umri wa miaka 16 lakini ni kinyume na sheria kupiga picha za ngono au kuchangia picha za ngono za kijana walio chini ya umri wa miaka 18.

Hata hivyo, ilisemekana kuwa vijana hawawezi kuchukuliwa hatua kwa kutuma picha zenye mada ya ngono miongoni mwao.