SIMBA, YANGA WAINGIZA SH. MILIONI 500

Mechi ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) ya watani wa jadi Simba na Yangailiyochezwa jana (Oktoba 20 mwakahuu) kwenye Uwanja wa Taifa, Dar esSalaam na kumalizika kwa sare ya mabao 3-3 imeingiza sh. 500,727,000.Washabiki 57,422 ndiyo waliokata tiketi kushuhudia pambano hilo namba 63kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 7,000, sh. 10,000, sh. 15,000, sh. 20,000na sh. 30,000.Ni tiketi 131 tu ndizo hazikuuzwa ambazo ni 90 za VIP A, 40 za VIP B namoja ya VIP C. Tiketi zilizochapwa kwa ajili ya mechi hiyo ni 57,558 ambayondiyo idadi ya viti vilivyopo kwenye uwanja huo.

Kila klabu imepata mgawo wa sh. 123,025,564.32 wakati Kodi ya Ongezeko laThamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 76,382,084.75.


Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 62,555,371.69, tiketi sh. 7,309,104, gharama za mechi sh. 37,533,223.01, Kamati ya Ligi sh. 37,533,223.01, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh.18,766,611.51 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh.14,596,253.39.