MWANAMKE MMOJA APIGWA RISASI BAADA YA KUKAIDI AMRI YA ASKARI

MWANAMKE mkazi wa PPF jijini hapa, Vailet Mathias, amepigwa risasi na polisi na kujeruhiwa eneo la Benki ya CRDB Mapato baada ya kukaidi amri halali ya Polisi na kumtishia silaha. Tukio hilo lilitokeajana saa 7 mchana katika benki hiyoya CRBD tawi la Mapato, mkabala naMamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) Mkoa wa Arusha.

Vailet alifika eneo hilo akiwa na gariaina ya Toyota Cresta namba T 888 BWW na kutaka kuliegesha katika lango la kuingilia magari ya kuchukua na kupeleka fedha katika benki hiyo.

Askari Polisi aliyekuwa akilinda eneo hilo, alimwamuru Vailet ambaye umri wake haukupatikana mara moja, kutoegesha gari eneo hilo, lakini akapuuza na kukaidi kisha akaingia ndani ya benki na hivyo askari huyo kuamua kutoa upepo kwenye matairi.

"Vailet alifika eneo hilo na kuingia ndani ya benki baada ya kupuuza amri ya askari aliyekuwa lindoni aliyemtaka atafute maegesho sehemu nyingine, lakini hakujibu kitu na kuwatazama askari waliokuwa hapo kwa dharau," alisema Kamanda wa Polisi wa Mkoawa Arusha, Liberatus Sabas alipokuwa anawathibitishia waandishi wa habari tukio hilo.

Alisema baada ya muda mfupi, Vailet alitoka nje na kukuta gari lakehalina upepo naye kwa hasira akamkabili askari Polisi aliyekuwa lindoni huku akimtolea maneno ya "hata kama una bastola nami ninayo" na kuitoa na kukoki akitaka amshambulie askari.

"Hata hivyo, askari alimwahi kwa bastola na kumpiga begani na kumfanya aanguke chini na bastola yake kumtoka mkononi," alisema Kamanda Boas huku akitoa mwito kwa wananchi kutii sheria bila shuruti. Alisema alichokifanya mwanamke huyo ni ukiukaji mkubwa wa sheria na kosa la jinai.

"Tunaomba kila mtu atii sheria, huuni ukiukwaji wa sheria na alimtishia bastola askari wetu, naye askari akamwahi maana eneo hili ni muhimu na hatujui mhusika alikuwana lengo gani," aliongeza Kamanda.

Mmoja wa mashuhuda wa tukio hilo, Fatma Kikuyu alidai mwanamke huyo alifanya kosa kukaidi amri ya Polisi na kuonesha ubabe kwa polisi na ndiyo maana tukio hilo likamkuta. Vailet alikimbizwa katika hospitali ya Mount Meru kwa matibabu, lakini alipofikishwa hapo alitolewa na kukimbizwa katika hospitali ya Selian.

Kwa mujibu wa taarifa za ndani ya hospitali hiyo kutoka kwa daktari, ambaye hakutaka kutaja jina lake, Vailet alifikishwa hapo na wakati huo alikuwa akisubiri kuingizwa katika chumba cha upasuaji ili kutolewa risasi iliyompata kwenye bega la kushoto.


Source:Habari leo