TCU YATOA ONYO KWA WANAFUNZI WANAODAHILIWA MOJA KWA MOJA NA VYUO

TAARIFA KWA UMMATume ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU) ina mamlaka kisheria kusimamia na kuratibu udahili wa Wanafunzi wote wanaojiunga na Vyuo Vikuu vyote nchini Tanzania.

Tume imebaini kuwa, hivi karibuni baadhi ya Vyuo Vikuu vimekuwa vikitangaza kudahili Wanafunzi moja kwa moja kupitia Vyuo vyao kwa mwaka wa masomo 2014/2015.

Ifahamike kuwa, utaratibu unaotambulika kisheria ni wa kudahili Wanafunzi kupitia Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania na si vinginevyo.

Hivyo mwanafunzi atakayeomba na kupatiwa udahili kupitia Chuoni moja kwa moja, udahili wake hautatambulika.

Tume inapenda kusisitiza kuwa waombaji wote wenye sifa za kujiunga na Vyuo Vikuu wanapaswa kufuata tartibu na miongozo iliyowekwa na Tume.

Taarifa hii imetolewa na KatibuMtendaji wa Tume ya Vyuo Vikuu.

Kwa mawasiliano zaidi, barua pepe es@tcu.go.tz na/au simu +255 222772657