JESHI LA POLISI ZANZIBAR LANASA RISASI 123

Katika hali ya kushangaza na kushtua jeshi la Polis mkoa wa kusini Zanzibar limefanikiwa kuzinasa risasi 123 za kivita ziliozkuwa ndani ya magazini nne ambazo zilkuwa ndani ya kisima huku ikiwakamata watu wawili kutokana na kuondoka na risasi hizo.

Kamanda wa Polisi mkoa wa kusini unguja kamishna msaiidzi Juma Saadi Khamis ambaye alifika kwenye tukio amethibitisha kupatikana kwa risasi hizo amabzo zilikuwa ndani ya magazini nne na zilikuwa zimezongwa ndani ya majani ya mgomba ambapo wachimba kisima waliokuwa wakikisafisha ndio walioziibua na kuzitoa ambapo awali hawakuzieelewa kama ni risasi ambapo mmoja yao mchimbaji Gefrey Silas amesema wao waliziweka juu na wakaja vijana wawili wakazichukua baadhi yake na ndipo wakatoa taarifa kwa Polisi jamii.

Akitoa maelezo ya ziada kamanda juma amewataja watu wawili Abdullah Suleiman na Mateo Makungu maarufu dilli wote wakazi wa kizimbani ambao walizichukua na kuzifikia eneo lengine huku akithibitisha risasi na magazine zote zimepatikana na upelelzi bado unaendelea huku risasi hizo zikionekana ni za muda.

Hili ni tukio la pili la Polisi kukamata shehena kubwa za risasi za vita katika kipindi cha miezi mitatu ambapo risasi hizo zimekutwa katika shamba linalomilikiwa na mmoja ya mwananchi na eneo hilo halina makazi ya watu ilawalinzi tu na kisimaa hicho kimekuwa hakitumiki kwa muda mrefu.