KIJANA APIGISHWA MBIZI KWENYE DIMBWI LA MAJI

Askari wa jeshi la Wananchi la Tanzania (JWTZ) akimwadhibu kijana ambaye hakuweza kufahamika jina lake mara moja, kwa kumpigisha mbizi kwenye dimbwi la maji ya barabarani baada ya kukutwa akiwa ametinga sare za Jeshi la Wananchi huku akipiga misele mitaani wakati akitambua kuwa yeye si askari ni raia wa kawaida.

Kijana huyo alikutana na adhabu hiyo kali kutoka kwa mjeda huyo baada ya kumbaini kuwa si askari halisi ya jeshi la Tanzania wakati alipokamatwa na kushindwa kutoa maelezo ya kuridhisha kuhusiana na swala zima la kijeshi, na hapo ndipo alipoanza kuamuliwa kuvua mavazi hayo na kisha kuaza kutumikia adhabu hiyo.

Tukio hilo lilitokea hivi karibuni maeneo ya Kariakoo jijini Dar es Salaam.