VODACOM WATOA TAARIFA JUU YA KUKATIKA NETWORK

TAARIFA KUTOKA VODACOM KUHUSU
TATIZO LA MTANDAO

Moto uliozuka leo katika mitambo ya
kuendesha mtandao (switch) wa
Vodacom umezimzwa jioni hii.

Akizungumza jioni hii Afisa Mkuu wa
Mawasiliano wa Vodacom, Georgia
Mutagahywa alisema moto huo
ulipelekea kusimama kwa huduma
zote za kampuni hiyo.

"Tunawaomba radhi wateja wetu wote
kutokana na usumbufu wa kukosa
mawasiliano uliosababishwa na
kuungua kwa vifaa muhimu vya
kuendesha mitambo yetu.

Ninapenda
kuwahakikishia kwamba wataalam
wetu wanafanya kila jitihada
kurudisha mawasiliano ya mtandao
wa Vodacom haraka iwezekanavyo,"