DAKTARI AIBA DAWA ZA KULEVYA AINA YA HEROINE TUMBONI KWA MGONJWA

Polisi nchini Urusi wamemzuilia
daktari mmoja mpasuaji kwa madai
ya kuiba kifuko kilichokuwa na dawa
ya kulevya ya Heroin kutoka tumboni
mwa mgonjwa.

Polisi katika eneo la Siberian
walimtaka daktari kumfanyia upasuaji
mshukiwa ili waweze kunasa dawa
hiyo ambayo mgonjwa alikuwa
ameimeza.

Hata hivyo polisi
waligundua kuwa seheme ya dawa
hiyo iliyotolewa tumboni mwa
mshukiwa ilikuwa inakosekana
Maafisa wa utawala wanadai kuwa
daktari huyo alikuwa mlevi
walipomkamata.

Huenda akafungwa
jela kwa miaka 15 ikiwa atapatikana na
hatia ya wizi wa dawa za kulevya.