FUNDI BAISKEL AMNAJISI MTOTO

Fundi baiskeli mmoja
mkaazi wa mtaa wa
Nsemlwa, wilaya ya
Mpanda, mkoa wa
Katavi, Athumani
Mussa (54) amefikishwa
jana katika Mahakama
ya Hakimu Mkazi ya
Wilaya ya Mpanda kwa
tuhuma za kumlawiti
(kunajisi) mdomoni
mtoto msichana (4)
baada ya kumdanganya
kumpatia mdoli wa
kuchezea.

Mtuhumiwa alifikishwa
mahakamani hapo na
kusomewa mashitaka na
mwendesha mashitaka
mkaguzi wa msaidizi wa
polisi Razalo Masembo
mbele ya Hakimu mkazi
mfawidhi wa Mahakama
ya Wilaya ya Mpanda
Chiganga Ntengwa.

Mwendesha mashitaka
aliiambia mahakama
kuwa mshitakiwa
Athumani Musa alitenda
kosa hilo Julai 24
mwaka huu majira ya
saa 12 jioni nyumbani
kwake katika mtaa wa
Nsemlwa mjini hapa.
Mtuhumiwa anadaiwa
kuwa siku hiyo ya tukio
alimwona mtoto huyo
akiwa na wenzake
wakicheza barabarani
karibu na
nyumbani kwake
ndipo alipomwita mtoto
huyo na kumwambia
amfuate nyumbani
kwake ili akampe mdoli
wa kuchezea. Mara
baada ya mtoto huyo
kuingia ndani,
mtuhumiwa alianza
kumnajisi mtoto huyo
mdomoni huku
akiwaamekaa kwenye
kochi lake sebuleni.
Ilidaiwa kuwa licha ya
mtoto huyo kupiga
mayowe ya kuomba
msaada, mtuhumiwa
hakujali mayowe ya
mtoto huyo bali
aliendelea na shughuli
yake hadi hapo
alipomaliza haja yake.

Mwendesha
mashitaka alidai kuwa
mtoto huyo alipotoka
nyumbani kwa
mtuhumiwa
alielekea nyumbani kwa
mama yake huku
akilia kwa sauti
kubwa, hali
iliyosababisha watoto
wenzake wamfuate kwa
nyuma.

Masembo alieleza mara
baada ya kufika kwa
mama yake na kuulizwa
analia nini, mtoto huyo
alitema mdomoni mbele
ya mama yake shahawa
akimweleza mama
yake alichofanyiwa na
fundi baiskeli, Musa.
Mama wa mtoto
huyo aliangua kilio na
kufanya majirani
wakusaniyike na ndipo
alipowasimulia mkasa
huo.

Majirani hao walichukua
jukumu la kwenda
kumkamata
mtuhumiwa wakiwa
wameongozwa na mtoto
huyo ambaye alikataa
kuingia ndani ya
nyumba ya mtuhumiwa
kwa kudai anaogopa
kunajisiwa tena na
mtuhumiwa.

Mtuhumiwa
Athumani Musa alikana
shitaka hilo na Hakimu
Mkazi Mfawidhi,
Chiganga Ntengwa
aliamuru mshitakiwa
apelekwe rumande hadi
Septemba 2 kesi yake
itakaposikilizwa.