MWINGINE ADAKWA NA DAWA ZA KULEVYA

Habari ambayo imeripotiwa naITV inadai kwamba baada ya siku moja ya ziara ya kushtukiza ya Waziri wa uchukuzi Dk. Harison Mwakyembe kwenye uwanja wa ndege wa kimataifa wa Julius Nyerere jijini Dar-es-Salaam, kiasi kikubwa cha dawa za kulevya kimekamatwauwanjani hapo katika harakati za kusafirishwa kwenda nchi zanje.

Aliekamatwa ni kijana ambae alikua anazisafirisha hizo dawa zikiwemo bangi pia akielekea nchini Italia.