JESHI LA POLISI LAKANUSHA UVUMI JUU YA SHEIKH PONDA KUPIGWA RISASI

Jeshi la Polisi mkoani Morogoro limekanusha kumpiga risasi Katibu wa
Jumuiya ya Taasisi za Kiislam Sheikh Ponda Issa Ponda.

Kamanda wa Polisi mkoani Morogoro ACP Faustine Shilogile amesema
polisi walikwenda kumkamata lakini kwa kusaidiwa na wafuasi wake
aliwatoroka na hawajui alipo. Jeshi hilo bado linamsaka na halina
taarifa kama yupo hai au la.