WANAFUNZI WANUSURIKA KUFA BAADA YA MABWENI KUTEKETEA

Zaidi ya wanafunzi mia moja themanini wa shule ya sekondari Engutoto wilayani Monduli mkoani Arusha wamenusurika kifo baada ya mabweni matatu kuteketea kwa moto usiku wa kuamikia leo na kuunguza vitu vyote yakiwemo madafutari nguo na vitabu huku vifaa vingine vikitajwa kuibwa na baadhi ya watu waliyokuwa wanawaoko wanafunzi hao.

Wakizungumza shuleni hapo wanafunzi waliyonusurika na tukio ilo wamesema tukio limetokea wakati wanafunzi hao wakiwa katika masomo ya usiku na kwamba moto huo umeteketeza kila kitu hawana nguo wala vifaa vya shule na wengine wanafanya mtihani mwaka huu hivyo wameiomba serikalki na wadau wawasaidie ili kuendelea na masomo.

Mkuu wa shule ya sekondari Engutoto Lomaiyan Sailep amesema hali ni mbaya hasa ukizingatia tukio ili limetokea ghafla lakini walimu na wadau wengine wanafanya mpango wa kutatua tatizo ilo.

Naye mkuu wa wilaya ya Monduli Jowika Kasunga amesema pamoja na kuwa tatizo ilo ni kubwa na lakusikitisha lakini binadamu wamekosa mtu kwani baadhi ya watu wameiba vifaa vya wanafunzi na kukimbia navyo lakini serikali itahakiksha inawatafuta watu hao samamba na kutafuta ufumbuzi ili watoto waendelee kusoma.