BOMU LA VITA YA PILI YA DUNIA LAPATIKANA UWANJA WA Borussia Dortmund

Signal Iduna Park


Bomu la vita vya pili vya dunia ambalo halijalipuka limepatikana katika uwanja wa Borussia Dotmund.

Bomu hilo lililoripotiwa na mwandishi wa DW nchini Ujerumani linadaiwa kuwa na chimbuko la Uingereza na sasa kuna mpango wa kulivunja makali.

Ugunduzi huo unajiri saa kadhaa kabla ya mkufunzi wa kilabu hiyo Jurgen Klopp kuzungumza na vyombo vya habari kabla ya mechi ya siku ya jumamosi na klabu ya Shalke.

Watu waliokuwa karibu na uwanja huo unaobeba takriban watu 80,720 waliondolewa.

Haijulikani ni kwa mda gani eneo hilo la uwanja litakuwa haliendeki walisema wamiliki wa kilabu hiyo waliofunga eneo la mashabiki pamoja na makazi ya kilabu hiyo.