MWANAMKE AMUUA MTOTO WAKE NA WATOTO WAWILI JIRANI YAKE

Mwanamke mwenye umri wa miaka 20 amemuua mwanae pamoja na watoto wawili wa jirani yake nchini Kenya.

Siku ya jumanne asubuhi Catherine Muthoni alimfungia ndani mwanae kabla ya kwendakuwashambulia watoto wawili wa jirani yake.

Kwa mujibu wa polisi na majirani wanasema kuwa mwanamke huyo alianza kumnyonga mtoto ambaye alikuwa na umri wa miaka 4 kabla ya kumuua mtoto mchanga wote wakiwa ni watoto wa jirani yake.

Inasemekana kuwa mama wa watoto hao alijaribu kuomba msaada wa kuwaokoa wanae lakini haikuwezekana maana alisukumwa na kuaguka chini huku akiugulia maumivu baadaya kutoneshwa sehemu alipofanyiwa upasuaji wakati wa kujifungua.

Polisi nchini Kenya wamesema kuwa chanzo cha tukio hilo akijajulikana lakini bado wanaendelea na uchunguzi mkali juu ya tukio hilo.