SERIKALI YAKANUSHA TUHUMA TOKA UN

Tanzania imekanusha vikali tuhuma kwamba imekuwa ikiwaruhusu viongozi wa kundi la waasi la FDLR kufanya mikutano nchini humo.

Hapo jana kulikuwa na taarifa ambazo zilitangazwa na vyombo mbali mbali vya habari duniani kuhusu ripoti mpya ya kundi la wataalamu wa umoja mataifa kuhusu Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo kwamba iilituhumu Tanzania kwa kuwaruhusu viongozi wa kundi la waasi FDLR kuandaa mikutano nchini humo.

Katika ripoti hiyo pia wanajeshi wa Burundi wanatuhumiwa kuwa walitekeleza unyanyasaji wa kingono.