ARSENAL WAMTEMA BROOKLYN BECKHAM

Brooklyn akiwa na ndugu zake Romeo na Cruz


Brooklyn Beckham, ambaye ni mtoto wa mwanasoka na nahodha wa zamani wa timu ya England, amebaki njia panda baada ya jaribio lake la kutaka kutetea udhamini wake na timu ya Arsenal.

Brooklyn mwenye umri wa miaka15, alikuwa akijihusisha na chuo cha timu hiyo cha Hale End academy na alikuwa na matumaini ya kupata mkataba wamiaka miwili kuendelea na washika bunduki hao.

Hata hivyo, imeelezwa kuwa kijana huyo hatakuwa chuoni hapo msimu ujao na hapo ndio atakuwa amemaliza mkataba wake na Arsenal.

Taarifa hii imekuja bila kutegemewa baada ya baba wa kijana huyo kupigiwa simu na klabu hiyo ya vijana walio chini yamiaka 18 mapema mwezi huu.

Imetanabahishwa kuwa kijana huyo wa Beckham alikuwa pekee kati ya walio na umri wa chini ya miaka 16 na chini ya miaka 17 kusalia klabuni hapo Hale End academy wakati wengine wote Al Kass kwenye michuano ya vijana huko Qatar.

Beckham atasalia kwenye klabu hiyo mpaka mwishoni mwa msimu na haijafahamika mara moja kama kijana huyo atatafuta klabu nyingine ya kuelekea.

Pamoja na uamuzi wa kutomsajili kijana huyo katika klabu ya Arsenal kocha wa vijana chipkizi bado anamhesabu kijana huyo kuwa na kipaji cha hali ya juu lakini wapo vijana wengine ambao wanamzidi kwa mbali katika safu ya kiungo ambayo ni ya juu klabuni hapo. Na wanamuona Brooklyn kuwa anaweza kucheza vizuri zaidi akiwa na klabu nyingine akiamua.

Watoto wengine wa Beckham Romeo na Cruz wako katika chuo hicho cha Hale End.

Cruz, mwenye miaka 10, naye anakuja juu zaidi ya nduguze kwenye sokana ameelezwa kuwa ana kipaji cha hali ya juu.