IS WAMCHOMA MOTO AKIWA HAI RUBANI WA JORDAN

Kuna video ambayo imesambazwa katika mtandao na kikundi cha kigaidi cha dola ya kiislam almaarufu kama Islamic State (IS) wakidai na kuonesha rubani mwenye asili ya Jordan Moaz al-Kasasbeh akichomwa moto angali hai.

Ingawa mpaka sasa video hiyo haijathibitishwa, inamuonesha mwanamume mmoja akiwa amesimama kwenye kizimba na anateketea kwa moto.

Video yenye kuonesha kisanga hicho iliachiliwa mtandaoni mwanzoni mwa wiki hii na kusambazwa katika mtandao wa Twitter, account ambayo hutumika kwa shughuli za kunadi matukio ya IS.

December katika utekelezaji uungaji mkono majeshi yenye muungano na Marekani walioko kwenye mapambano na IS.

Nayo Runinga ya nchi ya Jordan imethibitisha kifo cha rubani huyo na kwamba alikwisha uawa mwezi mmoja uliopita.

Naye ndugu wa karibu wa Rubani Luteni Kasasbeh, aliliambia shirika la habari la Reuters kwamba wanajeshi wa Jordani waliiarifu familia ya Rubani huyo juu ya kifo chake.

Mwandishi wa BBC Frank Gardner ameielezea video hiyo kwamba ina lengo la kuwatisha watu, lakini pia ameeleza kuwa majeshi ya muungano na Marekani na hasa kikosi cha anga kimewaathiri vilivyo IS ,na IS wameonesha udhaifu wa dhahiri na kushindwa kwao na majeshi hayo.

Video hiyo imeelezwa kuwa na urefu wa dakika 22 inamuonesha Rubani huyo akitembea kwenye mvua ya risasi zilizokuwa zinatokea kwenye kikosi cha majeshi ya shirikisho yaliyokuwa yamewalenga wapiganaji hao.

Serikali ya Jordan ilijitahidi kadiri ya uwezo wake ili kumuokoa Luteni Kasasbeh kama mateka kwa kubadilishana na wafungwa,nayo serikali ya Jordan ilikuwa tayari kumwachilia huru Sajida al-Rishawi, ambaye alihukumiwa adhabu ya kifo nchini Jordan akihusishwa na uripuaji mabomu katika hoteli katika mji wa Amman mnamo mwaka 2005, kwa nia ya kubadilishana na wamuachilie Luteni Kasasbeh.

Kufuatia kutekwa kwa Rubani huyo, Familia na jamaa zake walikuwa wakikutana kila siku katika viunga vya nchi hiyo umbali mfupi kutoka katika kasri la kifalme la Amman.

Lakini inasemekana kwamba video hiyo imetolewa siku tatu baada ya ile ya kwanz ayenye kuonesha maiti ya mateka wa Kijapani Kenji Goto.