MKUU WA KITUO NJOMBE ATUPWA JELA MIAKA 30 KWA KUMBAKA MAHABUSU

Mkuu wa Kituo cha Polisi Njombe ahukumiwa kifungo cha miaka 30, kwa kumbaka mahabusu.

Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa ya Njombe, imemhukumu aliyekuwa mkuuwa kituo cha Polisi Ilembula kifungo cha miaka 30 jela,baada ya kukutwa na hatia ya kumbaka mtuhumiwa aliyekuwa ndani ya mahabusu.

Hukumu hiyo ilitolewa na Hakimu Augustine Rwezile, baada ya mshtakiwa huyo James Nyambenga kukiri kosa hilo mahakamani ambapo mshtakiwa huyo anadaiwa kumtoa msichana huyo kwenye chumba cha mahabusu alikokuwa anashikiliwa na kumbaka.

Mwanamke huyo ambae ni mhudumu wa baa alikuwa anashikiliwa kwenye mahabusu ya kituo hicho kwa tuhuma za uzururaji.

Akisoma hukumu hiyo Hakimu Rwezile amesema ushahidi uliotolewa na upande wa mlalamikaji na vielelezo vya daktari aliyempima msichana huyo viliweza kuithibitishia Mahakama kuwa mtuhumiwa alitenda kosa hilo.

Chanzo: Nipashe