MKURUGENZI MAMLAKA YA BANDARI ASIMAMISHWA KAZI

Waziri wa Uchukuzi Mhe. Samuel Sitta amemsimamisha kazi Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Bandari nchini (TPA), Eng Madeni Shamte Kipande kwa tuhuma za utendaji mbovu ikiwa ni pamoja na kutokuwepo kwa uwazi kwenye mamlaka hiyo hususa ni katika michakato ya zabuni mbalimbali zinazotangazwa na mamlaka hiyo.

Pamoja na kuchukua uamuzi huo Mhe. Sitta ameunda tume ya watu sita itakayokuwa na jukumu la kuchunguza tuhuma zinazomkabilia Mhandisi Kipande ambaye atakuwa nje ya madaraka kwa muda wa wikimbili kupisha uchunguzi huo nanafasi yake itakaimiwa na Meneja wa Bandari ya Dar es Salaam Bw. Awadhi Masawe.

Kipande aliteuliwa kushika wadhifa huo mwaka 2012 mwezi Agosti na aliyekuwa Waziri wa Wizara hiyo Dk Harrison Mwakyembe.