RAIS MUGABE AWASIMAMISHA WALINZI 27 BAADA YA KUANGUKA

Rais Mugabe akiwa na rais mpya wa Zambia Edgar Lungu

Taarifa kutoka nchini Zimbabwe inaarifu kwamba walinzi 27 wanaomlinda Rais Robert Mugabe wamesimimishwa kazi kwa kudaiwa hawakuwa wamejipanga baada ya rais huyo kuanguka chini.

Kwa mujibu wa vyanzo vya habari hii inasemekana walinzi hao walipewa barua za kusimamishwa kazi Ijumaa iliyopita.

Kuna ripoti pia kuwa baadhi ya maofisa wanaweza kufukuzwa kazi kutokana na mkasa huo.

Sura mpya za walinzi zilionekana siku ya ijumaa wakati Mugabe alipokutana na rais mpya wa Zambia Edgar Lungu mjini Harare.