WATU WAWILI WAUAWA KWA BOMU KABUL

Watu wawili wameripotiwa kufa na wengine wengi kujeruhiwa baada ya mlipuko kutokea kwenye uwanja wa kimataifa wa ndege katika mji mkuu wa Afganistan Kabul.

Walioshuhudia wanasema kuwa mlipuaji wa kujitolea mhanga alikuwa amelenga wanajeshi wa kimataifa nje ya lango kuu la uwanja huo wa ndege.

Haijabainika iwapo walikwepa shambulizi hilo au la.

Lango hilo hutumika na maafisa wa kijeshi wa kigeni pekee yao.

Msemaji wa polisi nchini humo amaiambia BBC kuwa shambulizi hilo lilifanyika karibu na afisi za halmashauri za safari za ndege nchini humo zilizoko nje ya uwanja wa ndege.

Mtu aliyeshuhudia alilitaja shambulizi hilo kuwa la kujitoa mhanga.

Shambulizi hilo linafanyika siku tatu baada ya mwanamgambo mmoja kuwaua watu 14 wakiwemo raia 9 wa kigeni mjini humo.