MTOTO ANAHITAJI MSAADA WA UPASUAJI NJIA YA HAJA KUBWA

FATIMA Msuya mwenye umri wa mwaka mmoja na miezi sita wa wilayani Namtumbo mkoa wa Ruvuma anahitaji kusaidiwa Sh milioni 2.5 ili afanyiwe upasuaji utakaowezesha kupata njia ya haja kubwa.

Mama wa mtoto huyo, Paulina Titus (48) alisema Fatima alizaliwa bila sehemu ya haja kubwa kabla ya kufanyiwa upasuaji kwa mara yakwanza katika Hospital ya Peramiho ambapo aliwekewa njia ya haja kubwa tumboni.

Paulina alisema hata baada ya kufanyiwa upasuaji huo, mtoto huyo hajaweza kujisaidia katika njia hiyo mpaka atakaporudi tena KCMC kwa upasuaji mwingine.

Aidha mama huyo alisema, kwa yeyote aliyeguswa na ambaye yupo tayari kumsaidia, atume msaada wake wa fedha kwa namba 0767 710113.